IBADA YA JUMAPILI 16/3/2014

            SOMO: KUBADILISHA VIWANGO KWA NGUVU YA ROHO WA MUNGU.
                                                   Pastor Sosthenes akihubiri

Tukumbuke kwamba Roho Mtakatifu amekuja ili tuishi maisha ya kufaa zaidi,maisha ya faida(profitable life),Yn 16:7-Bwana alisema yawafaa mimi niondoke,maana yake itatufaidia Roho akija.
-Yeye humtoa mtu mavumbini yaani humbadilishia mtu viwango toka chini kwenda juu.
1Samweli 2:6-8
-Anapokuja juu yako mabadiliko hutokea,vizuizi huondolewa mbele yako,unapiga hatua moja baada ya nyingine.
Isaya 32:15
-Mungu atakubeba kwa mbawa kama tai kukupeleka viwango vya juu.
Kutoka 19:4
 
Mchungaji akiendelea na mahubiri


JINSI YA KULIFANYA HILI LIWE HALISI

1. KUZALIWA MARA YA PILI
Huu ni mwanzo wa safari ya hatima njema ya mtu.Bwana alimwambia Nikodemo....hamna budi kuzaliwa mara ya pili-you must be born again-Yohana 3:7
Unapookoka yasiyowezekana yanawezeka,Mungu anatangulia mbele zako.Isaya 45:1-3.
Kuanzia leo naona Mungu akitangulia mbele zako!
Mungu anakufanya mzao mteule,taifa takatifu,mtu wa milki ya Mungu,ukuhani wa kifalme.1Petro 2:9-Ni vema uanze kujiita Mungu anavyokuita,anza kujiona Mungu anavyokuona.

2.JIONE UNAYO HATIMA NJEMA-SENSE OF DESTINY.
Kuna mahali kwa ajili yako! Ni mahali alipo kutengenezea Mungu kwa ajili yako. Kutoka 23:20.
Mawazo yake kwako ni kukupa mwisho mzuri tena wenye matumaini,kwanini usiwaze hivyo?
Warumi 8:29-30
Yeremia 29;11
Pata picha njema ya mwisho wako huo kupitia Neno la Mungu na kamwe hutakata tama.
Yesu Bwana wetu alipouona mwisho wake wa utukufu alidharau aibu na kuustahimili msalaba.Kila unapopata picha hiyo,utapiga mbio kuelekea hatima hiyo bila kuchoka.Waebrania 12;2-3

       Mchungaji akiwaongoza walioamua kumpa Yesu maisha yao,waliosimama nyuma ni wazee wa kanisa.
                                                             Mchungaji akiongoza maombi.
                                                                Kipindio cha maombi.
   
                                               Kwaya ya kina mama ikihudumu.

Comments