IBADA YA JUMAPILI 6/4/2014
SOMO: NGUVU ILIYOPO KATIKA UTOAJI
Somo hili litatoa maarifa kuhusu:
-kuwa na mtizamo sahihi kuhusu utoaji
-kutoa kwa namna iliyo sahihi
-mahali sahihi pa kutoa
-aina mbalimbali za utoaji
-dhawabu za utoaji
-msukumo katika utoaji
-nini cha kufanya kati ya utoaji na kuiona dhawabu ya utoaji wako.
-Mungu anayo sadaka yake.Anasema...mtatwaa kwake sadaka yangu.
-Utoaji
ni lango la
kuingia katika ulimwengu wa roho. Kama unataka mbingu zako ziwe
wazi,kama unataka mbingu zako zizungumze basi utoaji ni jambo lisilo
epukika.
-kila mmoja anahitaji msaada toka juu-Zaburi 60;11,utoaji utafungulia msaada huo.
-unapokuwa
umeshambuliwa na roho ya uchoyo na ubahili,mahangaiko hayawezi
kukuondokea.Bwana alisema jilindeni na choyo-Luka 12:15.
Naona roho hizi
zikiachia maisha yako katika jina la Yesu
-katika kila mapato yako,kuna mkate na mbegu.2Korintho 8:10;Kutoka 25:2
-Ni hekima kutambua mbegu katika kila pato lako kwa kuwa mbegu:
-Itatunza uzao au mtiririko(flow) wa mapato yako
-Itakuletea mazidisho.Mwanzo 26:12-14
-Hivyo mbegu bora itakuletea matokeo bora.
Kanisa la Makedonia lilijazwa na ukarimu na umaskini haukuwa na nguvu kwao.Ukarimu wao ulijengwa katika
misingi mikuu miwili.
1.Walijitoa kwa Mungu
2.Walijitoa kwa watumishi wa Mungu.
kwa kufanya hivi waliweza kutoa kwa uwezo wao na zaidi ya uwezo wao.
Comments
Post a Comment